Proverbs 7:1-6

Onyo Dhidi Ya Mwanamke Mzinzi


1 aMwanangu, shika maneno yangu
na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.

2 bShika amri zangu nawe utaishi;
linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.

3 cYafunge katika vidole vyako;
yaandike katika kibao cha moyo wako.

4 Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”
uite ufahamu jamaa yako;

5 dwatakuepusha na mwanamke mzinzi,
kutokana na mwanamke mpotovu
na maneno yake ya kubembeleza.


6 Kwenye dirisha la nyumba yangu
nilitazama nje kupitia upenyo
kwenye mwimo wa dirisha.
Copyright information for SwhKC